Saturday 13 January 2007

FAIDA ZA KUWA MWANACHAMA WA SACCOS.

Mwanachama baada ya kutimiza wajibu wake kama inavyoelezwa katika kipengele namba 2 cha kijitabu hiki atapata fursa ya kushiriki mikutano ya Chama,kushiriki semina za mafunzo katika kumjengea uelewa zaidi wa taratibu za kutunza akiba na mikopo na atapata fursa ya kukopa.

Ieleweke kwamba mikopo kwa wanachama itatolewa kuzingatia akiba yake ndani ya Chama na ambapo mkopaji atakopeshwa si zaidi ya mara tatu ya akiba yake chamani.

Inawezekana mwanachama akawa na hisa zake ndani ya chama na asihitaji kukopa huyu atapata gawio toka katika faida itakayopatikana kulingana na hisa zake baada ya mahesabu ya mwaka.

AINA YA MIKOPO ITOLEWAYO

-Biashara.
-Kilimo na Mifugo.
-Elimu.
-Maendeleo
-Dharula,jamii.
-Dharula,Biashara
-Mazao makavu (stock)

No comments: