Saturday 13 January 2007

DHAMANA YA MIKOPO.

Mwanachama atakuwa na haki ya kukopa ama ilivyoelezwa awali isipokuwa lazima adhaminiwe na wanachama wawili,ambao nao wana sifa ya kuwa wakopaji.

Wadhamini hao watamdhamini mkopaji kwa kujaza fomu maalumu iliyoandikwa na Bodi ya SACCOS na kutia sahihi zao.

La muhimu zaidi wadhamini wawe tayarikuhakikisha mkopo unarejeshwa kwa wakati kama ilivyoelezwa katika kipengele namba 5.

Wanachama watapatiwa semina kujua wajibu wao,viongozi watapatiwa semina za kuwajengea haki ipasavyo,ambapo wafanya kazi wa SACCOS watapatiwa mafunzo ya kuendesha shughuli za ki fedha na za ki benki.

Semina na mafunzo hayo yatafadhiliwa na CRDB Benki ltd.

No comments: