Saturday 13 January 2007

MUDA WA KUREJESHA.

Mkopaji atawajibisha kurejesha mkopo kwa kuzingatia mkataba na aina ya mkopo,kutakuwa na marejesho ya kidogo kidogo kila
wiki au mwezi,na muda wa kukaa na mkopo utakuwa kati ya mwezi mmoja,miezi 3,miezi 6,na mwaka mmoja.Bodi na kamati ya
mikopo itapendekeza na kufikisha katika mkutano mkuu,hatua za kuchukua mkopaji aliyechelewesha mkopo.

KUMTAMBUA MWANACHAMA.

Kila mwanachama atajaza fomu ya kujiunga na ataweka sahihi katika kitabu cha wanachama na picha yake.Pia atapewa
kitambulisho na kitabu cha fedha.

SALAMU ZA MWENYEKITI WA BODI.

Natumia fursa hii kueleza kwamba SACCOS hii imeanzishwa kwa ridhaa ya Wanachama wa TCCIA na wakazi wa Tabora waliokutana
katika mkutano wa kwanza,na wa pili uliopitisha Katiba tarehe 10.02.2006
Pia ieleweke kwamba kila Mwanachama anayo haki ya kuwa kiongozi wa SACCOS hii,kwa ridhaa ya wanachama,kwa msingi huo
SACCOS hii ni mali ya wanachama wote,kwa mujibu wa Katiba.
Hivyo nia na madhumuni ya SACCOS inaeleweka vizuri ndani ya KATIBA na SERA ambazo zipo katika ofisi za SACCOS,kwa
kifupi lengo kuu ni kumwinua mkazi wa Tabora kimtaji,kiuchumi,ki elimu na maendeleo ya mkoa wetu na kadhalika.

Nawaomba wakazi wa Tabora wajiunge na SACCOS hii ili tujenge misingi imara ya maendeleo ndani ya Tabora.Kwani yote hayo
yaliyofafanuliwa hapo juu yatawezekana kwa kushirikiana.La muhimu zaidi ukikopa tafadhari lipa kwa wakati na katika kujiunga
usisubiri kuhadithiwa.Ukitaka kujua uhondo wa ngoma ingia ucheze.

VIONGOZI WA BODI YA SACCOS.

1. WILLIAM MASUBI -MWENYEKITI WA BODI
2. DICK MULIMUKA -MAKAMU MWENYEKITI WA BODI
3. JOHN L.MCHELE -MWENYEKITI BODI YA MIKOPO
4. MARY D.MANYANGA-MJUMBE WA BODI
5. FRANK MGONJA -MJUMBE WA BODI
6. ZAKAYO MAGANGA -MJUMBE WA BODI
7. MICHAEL MAMBO -MJUMBE WA BODI
8. GULAM H.DEWJI -MJUMBE WA BODI
9. PETRONELA LYIMO-MJUMBE WA BODI

KAMATI YA USIMAMIZI.

1. PAUL B.MATOBOGOLO
2. AMANI MRISHO MAKUNGU
3. ANDREW KISHIKI

MENEJA WA SACCOS.
LAURENCE B. KASALA.

TIMIZA WAJIBU TABORA YENYE NEEMA INAWEZEKANA

ANWANI KAMILI.
TCCIA TABORA SACCOS LIMITED
LUMUMBA STREET
S.L.P 658 SIMU 026 260 4169
REG NO. 578
BARUA PEPE (E-MAIL) tcciatabora@yahoo.co.uk
TOVUTI (WEBSITE) http://tabora-saccos-ltd.blogspot.com
TABORA-TANZANIA

No comments: